Maalim Seif kutinga Mahakama ya ICC leo au kesho


Katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF, Maalim Seif Sharif Hamad amekuwa na ziara nje ya nchi tangu baada ya uchaguzi mkuu wa marudio Zanzibar March 2016 kuisha, Maalim Seif amekuwa akienda jumuiya za kimataifa kwa ajili ya kutafuta kile anachokiita haki kutokana na uchaguzi mkuu wa Zanzibar October 2015 kufutwa.
Leo July 21 2016 Naibu katibu mkuu wa chama cha wananchi CUF, Nassor Mazrui amekutana na waandishi wa habari ambapo aliulizwa mchakato wa kufungua kesi katika mahakama ya kimataifa ya ICC ili kudai haki yao kama walivyosema hapo awali.
Mazrui amesema kuwa leo au kesho Maalim Seif anatarajiwa kufika katika mahakama ya kimataifa ya ICC, The Hague nchini Uholanzi katika harakati zake za kudai haki katika uchaguzi uliofanyika october 2015…….
>>>’naamini kama si leo au kesho Maalim Seif atakuwa the Hague kwenda kuelezea namna gani demokrasia ya Zanzibar na Tanzania inavyominywa kwa hivyo suala la ICC tumelipania na lazima hiyo kesi itakwenda na kila aliyedhulumiwa, aliyedhulumu atafika katika mahakama ya ICC
Previous
Next Post »