Beenie Man aahirisha show ya OVO Fest baada ya kupata virusi vya Zika



Staa wa muziki wa Dancehall kutoka Jamaica, Beenie Man amelazimika kuahirisha safari yake ya Canada baada kupata maambukizi ya virusi vya Zika.
Beenie Man alitakiwa kutumbuiza kwenye show ya OVO Fest baada ya kunyimwa visa ya kuingia nchini humo baada ya vipimo vya damu kuonesha alikuwa na virusi vya Zika.
Beenie-Man
Baadaye alishare picha akiwa anafanyiwa vipimo na kuandika “No visa fi mi Canada show. The same Zika mosquito gi mi dengue. Blood test, injections, pills. Wi a hol firm still.”
Virusi vya Zika huambukizwa iwapo utang’atwa na mbu aliyemng’ata mwathirika wa virusi hivyo, au kwa njia ya ngono huku 80% ya waathirika wa virusi hivyo hawaoneshi dalili zozote za ugonjwa.
Previous
Next Post »