Watafiti wadai aina hii ya mende wanatoa Maziwa yenye protini kuliko ya ng’ombe


Moja ya yalioandikwa ni huu utafiti kwenye gazeti la Mwananchi yenye kichwa ‘Maziwa ya mende yana protini kuliko ya ng’ombe’
Uchunguzi wa wanasayansi umebaini maziwa ya mende yana virutubisho ya protini mara nne zaidi ya ng’ombe. Taarifa ya timu hiyo ya kimataifa ya wanasayansi hao ya ‘Institute of Stem Cell Biology and Regenerative Medicine’ ilisema maziwa hayo yanaweza kuwa muhimu kuwalisha watu wanaoongezeka duniani siku za usoni.
Sehemu ya taarifa hiyo ambayo imenukuliwa na mashirika mbalimbali duniani imesema……>>>’Ingawa mende wengi hawatoi maziwa, mende aina ya Diploptera punctute, wameonekana kutoa utomvu unaoonekana kama maziwa yenye protini yanayotumika kuwalisha watoto’

Taarifa hiyo imesema wadudu nao hutoa maziwa lakini kilichowashangaza zaidi watafiti ni yana nguvu mara tatu zaidi yanayopatikana kwenye maziwa ya kifaru.
Previous
Next Post »